.
12th September, 2016
Siku nne tu baada ya ndege mbili kuanguka Nairobi na Naivasha, mapema leo ndege nyengine imeanguka katika msitu wa Kibiku eneo la Ngong. Ndege hiyo ilikuwa ya kufanyia mazoezi ya urubani ikiwa na mkufunzi na mwanafunzi wake. Ajali hiyo ilimwacha mkufunzi huyo na mwanafunzi wake na majeraha madogo. Wawili hao walikimbizwa hospitalini kwa matibabu. Ndege hiyo iliyokuwa ikitoka uwanja wa ndege ya Wilson kwa ajili ya mafunzo inasemekana kuwa na hitilafu za mtambo kwenye injini. kulingana na OCPD wa Kajiado kusini George Seda mabaki ya ndege hiyo yatasalia hapo hadi uchunguzi utakapokamilika