Riadha za mchujo za kimataifa kufanyika Nairobi
2nd June, 2016
Majaribio ya riadha ya kitaifa ya kuchagua kikosi cha kushiriki michezo ya olimpiki jijini Rio huenda yakafanyika jijini Nairobi na wala sio mjini Eldoret kama ilivyopangwa hapo awali. Hii ni baada ya uwanja huo kutofikia hadhi inayostahili kuwa mwenyeji wa mashindano hayo. Shirikisho la michezo ya olimpiki nchini kilikuwa kimetangaza majaribio ya kitaifa yangefanyika mjini eldoret kufuatia mkutano kati ya shirikisho la riadha magavana wa kaunti ya Uasin Gishu na ya Elegeyo Marakwet Jackson Mandago na Alex Torgos mtawalio. Maafisa wa shirikisho la olimpiki wakiongozwa na mwenyekiti Kipchoge Keino na vile vile mwenyekiti wa riadha nchini Jackson Tuwei walizuru uwanja huo na kupata kuwa kazi iliyofaa kumalizika kabla ya majaribio bado haijafanyika. Mashindano ya majaribio ya kitaifa yatafanyika tarehe 29 na tarehe 30 wezi huu.