Clement Lang'at akita kambi nchini kujianda kwa mbio za Olimpiki huko Rio
12th May, 2016
Mshindi wa Nishani ya fedha katika mashindano ya Dunia ya mbio za Nyika Clement Lang’at amejiunga na wanariadha wanaojiandaa katika eneo la Bonde la Ufa kwa mashindano ya Olimpiki yatayoandaliwa nchini Brazil mwezi Agosti. Lang’at ameacha makazi yake nchini Japan ili kuja kufanya mazoezi nchini Kenya na ana matumaini kuwa atajumuishwa katika kikosi ili aiwakilishe Kenya katika mbio za Mita 5000. Mshindi huyo wa mbio za Nyika barani Afrika mwaka 2012 amekuwa akitatizwa na jeraha lilomweka nje kwa muda wa miaka miwili. Mara ya mwisho Kenya kushinda dhahabu katika mbio za Mita 5000 ilikuwa katika mashindano ya riadha ya Dunia mwaka 2005.