21st May, 2020
Baada ya miezi kadhaa ya shutma, rais wa shirikisho la soka nchini Nick Mwendwa ameitwa katika afisi kuu ya idara ya upepelezi nchini kuelezea kuhusiana na madai ya utumizi mbaya wa fedha.
Shirikisho hilo limeshtumiwa kuzifuja shilingi milioni 244 wakati wa dimba la AFCON mwaka 2019. Aliyekuwa katibu mkuu wa wizara ya michezo nchini Peter Kaberia pia alikuwa na duku duku la jinsi shilingi milioni 4 zilivyotumiwa wakati wa mechi za mchujo.
Suala la gari la matangazo ya nje lililogharimu shilingi milioni 125 ambalo mpaka sasa halijaonekana nchini pia ni moja ya shutma dhidi ya Mwendwa.