7th February, 2022
Wanaounga mkono Azimio la Umoja kaunti ya Kwale wamempuuza Naibu wa Rais William Ruto na mrengo wa Kenya Kwanza, wakisema kwamba chama cha ODM bado kina umaarufu katika kaunti hiyo. Wakiongozwa na mwenyekiti wa ODM kaunti hiyo Hassan Mwanyoha, wamewashauri wananchi kuwa makini wasipotoshwe na wanasiasa.