7th February, 2022
Huku wafanyakazi wa umma wakitakiwa kujiuzulu kwa nyadhifa za uongozi, katibu mkuu wa chama cha walinzi binafsi Isaac Andabwa ambaye pia anahudumu kwenye mamlaka ya kudhibiti ulinzi binafsi kwenye ofisi ya rais ni miongoni mwa wanaopanga kujiuzulu. Andabwa ambaye amekuwa mstari wa mbele kupigania haki ya walinzi wa binafsi nchini amesema kuwa analenga kutumia fursa hiyo kupigania haki ya wakenya wa tabaka la chini kule bungeni. Andabwa anamezea mate kiti cha ubunge cha Lugari