7th February, 2022
Rais Uhuru Kenyatta anatarajiwa kuzindua rasmi mpango wa huduma za afya kwa wote katika hospitali ya Port Reiz kaunti ya Mombasa ikiwa ni mojawapo ya hatua kuu ya kuimarisha afya kwa wakenya. Kuanzia mwaka wa 2018, serikali kupitia kwa wizara ya afya ilizindua jaribio la afya kwa wote kwa kipindi cha mwaka mmoja katika kaunti nne zilizochaguliwa kwa misingi ya ukubwa wa kaunti hizo, magonjwa yanayoambukizwa na pia vifo vya watoto wadogo.