9th December, 2019
Baadhi Ya Viongozi Wa Kanisa Kutoka Eneo La Bisil Katika Kaunti Ya Kajiado Wamejitokeza Kutoa Kauli Yao Kwa Makanisa Yote Humu Nchini Kuombea Taifa Na Mvua Ya Masika Inayoendelea Kunya Katika Maeneo Kadhaa Humu Nchini. Wakiongozwa Na Kasisi Daniel Osoi Wa Kanisa La Faith Evangelical, Wameomba Kuwepo Kwa Mvua Ya Wastani Ambayo Haitasababisha Maafa Na Hasara Kubwa Kama Ilivyoshuhudiwa Hivi Majuzi. Wakizungumza Katika Hafla Ya Kutawazwa Kwa Makasisi Wamewafariji Wale Waliopoteza Wapendwa Wao. Aidha Wametoa Wito Kwa Serikali Kuhakikisha Kwamba Imeandaa Mikakati Ya Kukabiliana Na Majanga Nchini.