9th December, 2019
Gavana Wa Kaunti Ya Nairobi Mike Sonko Amefikishwa Mahakamani Leo Hii Kushtakiwa Kwa Tuhuma Za Ufisadi Na Matumizi Mabaya Ya Ofisi Yake. Upo Wasi Wasi Mkubwa Wa Pengo Katika Uongozi Wa Kaunti Ya Nairobi Ikizingatiwa Kuwa Gavana Sonko Hana Naibu. Baraza La Magavana Hata Hivyo Limemtaka Rais Uhuru Kenyatta Kuandaa Kikao Cha Dharura Kuliangazia Suala Hilo Na Kuondoa Shaka Ya Siku Za Usoni Iwapo Tukio La Aina Hiyo Litatokea.