5th November, 2018
Jopo la majaji watano linaanza hivi leo kusikiliza kesi ya ufisadi na matumizi mabaya ya mamlaka inayomwandama Naibu Jaji mkuu Philomena Mwilu.Jaji mkuu David Maraga alibuni jopo hilo baada ya kesi hiyo kuwasilishwa kwake kufuatia ombi la kiongozi wa mashtaka ya umma Noordin Haji.***************katika ombi lake kiongozi wa mashtaka alisema kesi ya Mwilu inazua maswala mazito ya kikatiba na inahitaji kusikilizwa na majaji zaidi ya mmoja. Majaji Chacha Mwita, Mumbi Ngugi, William Musyoka, Francis Tuiyott na Hellen omondi watasikiliza kesi hiyo. Jaji Philomena Mwilu ambaye alikamatwa tarehe 28 mwezi Agosti na kufikishwa mahakamani anapinga hatua ya kumfungulia mashtaka kuhusiana na madai ya ukwepaji kulipa kodi na kutoa rushwa.