17th September, 2018
Wakazi wa kambi ya juu huko isiolo wanaishi maisha ya kuogopa kufuatia ongezeko la visa vya uhalifu eneo hilo. watu watatu wameuawa eneo hilo katika muda wa mwezi mmoja, kisa cha hivi punde ni kuuawa kwa mwanamke mmoja kisha kutolewa kwa viungo mwilini mwake. Naibu kamishina wa kaunti ya isiolo Robert Wangila amewalaumu wenyeji kwa kutotoa taarifa muhimu kuhusiana na mashambulizi ya kila mara kwa mara na kulemaza juhudi za maafisa wa usalama kuwasaka wahusika.