22nd August, 2018
Leo Kenya inaadhimisha miaka 40 tangu kufariki kwa mwanzilishi wa taifa la kenya Mzee Jomo Kenyatta agost 22 mwaka wa 1978. Ukumbusho wake mwaka huu unafanyika wakati kuna mwamko mpya na pia shauku ya kisiasa iliyoletwa na salamu za heri kati ya rais uhuru kenyatta na kiongozi wa upinzani raila odinga.lakini je, wafahamu kuwa kulikuwa na hali kama hiyo miaka 40 iliyopita? Mzee jomo kenyatta na babake raila odinga jaramogi oginga odinga walifaa kusalimiana kwa heri siku moja kabla ya kifo cha jomo kenyatta kama anavyokariri binamu yake rais uhuru kenyyata Jomo Kenyatta Ngegi Muigai.