17th April, 2018
Mwanamke mmoja anazidi kupokea matibabu katika hospitali ya Migori baada ya kupokea kichapo kutoka kwa mumewe kwa madai amekuwa na uhusiano wa mapenzi na muhudumu wa bodaboda. Sophie Maroa mwenye umri wa miaka 33 amesema mumewe alianza kumpiga baada ya kumlimbikizia madai hayo. Aidha aliwaambia wanahabari kwamba kwa miaka nyingi tu amekuwa akipitia mateso kutoka kwa mumewe ila akayanyamazia. Wahudumu wa afya katika hospitali hiyo wanasema mara nyingi wanapokea visa vya aina hiyo ila wengi wanaogopa kuripoti kujikinga na dhuluma zaidi.