.
4th March, 2012
Watu watano wa familia moja wamepoteza maisha yao papo hapo huko Mwea katika ajali mbaya ya barabarani. Ajali hiyo katika barabara ya makutano- Embu ilitokea pale gari ndogo lilipogongana ana kwa ana na basi moja lililokuwa njiani kuelekea Meru kutoka Nairobi. Na katika ajali nyingine mbaya, huko kaunti ya Bungoma, wanafunzi 10 wa shule kadhaa katika kaunti ya Bungoma walifariki, baada ya lori moja kuwagonga walipokuwa wanatembea kutoka mashindanoni.