3rd January, 2020
Seneta Wa Busia Amos Wako Ameungana Na Viongozi Wengine Kutoka Magharibi Ya Kenya Kupuuzilia Mbali Mkutano Uliopangwa Kufanyika Katika Uwanja Wa Bukhungu Mjini Kakamega. Wako Amedai Kwamba Katibu Mkuu Wa COTU Francis Atwoli Hajashauriana Na Viongozi Wa Eneo Hilo Kuhusu Mkutano Huo, Unaonuiwa Kuzungumzia Mwelekeo Wa Ripoti Ya Bbi. Ameelezea Hofu Yake Kwamba Mkutano Huo Huenda Ukatumika Kuwagawa Waluhya Hata Zaidi.
Kwa Upande Wake Francis Atwoli Amekanusha Vikali Madai Ya Bi Alice Wahome Akisema Kuwa Yeye Ni Kiongozi Wa Muungano Wa Vyama Vya Wafanyakazi Na Hana Majukumu Yoyote Katika Shughuli Za Serikali. Alizungumza Huko Nakuru.