28th September, 2018
Huenda kampuni ya sukari ya Transmara iliyoko eneo la Kilgoris ikalazimika kufunga operesheni zake kufuatia madai ya kuharibu mazingira na kuchafua chemichemi za maji.
Hii ni baada ya kamati ya kuangazia malalamishi ya mazingira kushuhudia uharibifu mkubwa unaoendelezwa walipozuru kampuni hiyo kutathmini hali baada ya malalmishi kutoka kwa wakaazi.