27th August, 2018
Gavana wa Mombasa Hassan Joho ameshutumiwa na baadhi ya viongozi wa eneo la North Rift kufuatia matamshi yake alipodai kwamba yeye ni rafiki ya rais uhuru kenyatta. Mbunge wa kapseret Oscar Sudi amesema kwamba kauli hiyo ya Joho ni kinaya na unafiki, huku akisema kwamba wanatazama kwa macho ya uangalifu jinsi matamshi fulani yanalenga kumdunisha Naibu Rais William Ruto.