27th August, 2018
Waumini wa kanisa la angilikana katika eneo la pokot magharibi wameandaa maandamano ya amani ili kushinikiza makao makuu ya kanisa hilo kuupa mji wa kapenguria hadhi ya dayosisi.
Wakibeba mabango wakristo hao waliandamana katika mji wa kapenguria huku wakiimba nyimbo za kulitaka kanisa hilo kuwapa dayosisi. Wanasema imepita miaka 24 sasa tangu wao kuanzisha mchakato wa kupewa dayosisi na hadi kufikia sasa malilio yao hayajasikizwa na yeyeote licha ya wao kufanya hima kufungua makanisa katika kaunti ya Pokot magharibi.