25th August, 2018
Baadhi ya viongozi kutoka Pokot wamekosoa vikali kura ya maoni ya shirika la IPSOS na kuhoji lengo kuu la kura hiyo lilikuwa ni lipi haswa kutokana na jinsi ilivyoangazia swala la ufisadi.
Wakiongozwa na Gavana wa Pokot magharibi profesa John Lonyangapuo pamoja na seneta wa eneo hilo Samuel Poghisio viongozi hao walishangazwa na jinsi orodha inayokisiwa ni ya wafisadi ilivyotolewa. Sasa wanataka shirika hilo lichunguzwe.