6th June, 2018
Juhudi za kutafuta ndege ya Fly Sax iliyopotea baada ya kutoka katika uwanja mdogo wa ndege wa Kitale zingali zinaendelea katika msitu wa njambini kaunti ya Nyandarua. Taarifa zinasema kuwa huenda ndege hiyo ilianguka katuika maeneo ya Kinangop. Mashirika mbalimbali yamo katika shughuli za pamoja kutafuta ndege hiyo. Maafisa wa halmashauri ya safari za anga, idara ya polisi, maafisa wa shirika la wanyamori na wadau wengine wanaendelea na juhudi hizo.