Hassan Joho amlaumu Marwa kwa masaibu yake
11th March, 2016
Hatua ya kuondolewa kwa walinzi wa viongozi kutoka pwani ya Kenya kuanzia Gavana Joho wa Mombasa ,naye kingi wa kilifi na sasa mbunge wa mvita Abdulswamad Shariff Nassir kunazua tumbo joto miongoni mwa muungano wa cord. Serikali inalaumiwa kwa kuwakandamiza viongozi kutoka pwani ya kenya wamelalamikia hatua hio na kusema hilo ni kurejesha wakenya nyuma na kuhatarisha maisha yao.