.
26th January, 2022
Baada ya Musalia Mudavadi kutangaza kujiunga na Naibu Rais William Ruto na hivyo kujiondoa katika muungano wa One Kenya Alliance, kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka sasa ndiye mwanasiasa anayetazamwa na wengi kwa sasa.
Wanachosubiri wengi ni kuona mkondo upi wa kisiasa ambao Kalonzo atauchukuwa. Je, atajiunga na vuguvugu la Azimio la Umoja la Raila Odinga ama ataamua kugombea mwenyewe urais katika uchaguzi mkuu wa agosti.
Na je, Kalonzo ana ushawishi upi wa kisiasa na idadi ipi ya wafuasi na wapiga kura?