.
15th January, 2022
Kinara wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka, leo amepata uungwaji mkono kutoka kwa jamii yake ya Ukambani kuwania urais mnamo agosti 9 mwaka huu. Akikubali idhini hiyo, Kalonzo amesema hakuna kile kitakachomzuia kuwania kiti cha urais, akiahidi kuondoa ufisadi, kuunganisha taifa na kuleta maendeleo nchini. Na kama anavyoarifu mwanahabari wetu wa masuala ya siasa Chris Thairu, kalonzo pia alikanusha madai kwamba atamuunga mkono kinara wa ODM Raila Odinga ambaye sasa ana chomba kipya cha vuguvugu la azimio la umoja.