24th December, 2021
Kwa zaidi ya miaka 50 wakazi katika bonde la kerio wamekuwa wakihangaishwa na matukio ya kila mara ya wizi wa mifugo. Visa hivi vimesababisha vifo vya watu wengi, kina mama kusalia wajane na watoto mayatima huku wengine wakilazimika kukatiza masomo yao kutokana na ukosefu wa usalama. Kando na usalama kwenye bonde la Kerio, maendeleo vilevile yameonekana kukwama kutokana na uchochole uliokita kambi katika baadhi ya maeneo baada ya mifugo kuibiwa. Na kwenye makala maalum ya makovu ya bonde la Kerio Elvis Kosgei anaangazia wajane waliofiliwa na wapendwa wao, watoto waliopoteza wazazi wao pamoja na wakazi waliolemazwa na wizi wa mifugo.