4th December, 2021
Vinara wa muungano wa “One Kenya Alliance, Kalonzo Musyoka na Musalia Mudavadi wamesema muungano huo uko imara na kuwataka wakenya kupuzilia mbali kile walichodai ni propaganda zinayoenezwa na wapinzani wao kwa kusudio la kuwagawanya. Vinara hao wametaka tume ya uchaguzi kuendeleza majukumu yake ya kuandaa uchaguzi mkuu mwakani bila ya kushurutishwa na upande wowote. Viongozi hao walizungumza baada ya kuhudhuria maombi katika kanisa la Nairobi East Seventh Day, mtaa wa Lunga Lunga, Nairobi.