.
4th December, 2021
Shughuli ya kuwaokoa wachimba migodi Abimbo kule Bondo, kaunti ya siaya bado inaendelea, huku ikiwa ni mmoja tu kati ya wanane walikuwa wamesalia katika shimo hilo akiokolewa akiwa hai. Livingston Odhiambo, mwanamume wa miaka thelathini na tisa na baba ya wanawe watatu akiokolewa usiku wa kuamkia leo, na wakati huo mwenzake akipatikana ameaga dunia. Shughuli ya uokozi unaendelea huku wasita wakiwa bado wamesalia katika mgodi huo wa dhahabu.