.
3rd December, 2021
Sasa ni rasmi kwamba wanafunzi katika shule ya sekondari ya wavulana ya Kakamega watalipa faini ya shilingi elfu tisa mia nane ishirini na tatu kila mmoja kugharamia hasara ya moto ulioteketeza bweni na kuharibu mali. Jaji wa mahakama kuu mjini Kakamega, William Musyoka, aliagiza kwamba ni lazima ada zote na malimbikizi yote ya karo zilipwe kikamilifu ndipo wanafunzi waruhusiwe kuingia shuleni. Na anavyoripoti, Shadrack Mitty, tayari mkuu wa shule hiyo, Gerald Orina, amewatumia wazazi na walezi waraka wa kuwaarifu utaratibu wa shule kufunguliwa tena.