.
3rd August, 2021
Kwa mara nyingine tena Seneta wa Baringo Gideon Moi, ameelezea matumaini yake kuwa mchakato wa kurekebisha katiba kupitia BBI, utarejeshwa na mahakama ili manufaa yaliyokusudiwa kuwafaidi raia yasipotee. Gideon Moi amekitaja kile kipengee kuhusu idadi ya maeneo bunge na kupeleka pesa mashinani, kuwa chenye manufaa zaidi kwani raia angepata maendeleo kwa haraka. Aidha amemrai Rais Uhuru Kenyatta kuendelea kuimarisha uchumi ambao umeathirika vikalikutokana na janga la korona. Seneta huyo alikuwa akizungumza huko ngata Nakuru, katika hafla ya mazishi ya Willie Kibichy Kipchillat, mfanyabiashara aliyekuwa rafiki ya familia.