.
1st June, 2021
Wafugaji wa kuku kaunti ya migori huenda wakanufaika pakubwa iwapo pendekezo la kujengwa kwa kiwanda cha kuku katika kipindi cha miezi mitatu litatekelezwa. Kiwanda hicho kimetajwa kitaboresha uchumi wa wafugaji wa kuku na kuwatoa katika hali ya uchochole. Gavana wa Migori Zachary Obado amesema serikali yake imejitolea kuboresha maisha ya wakulima mashinani kupitia miradi ya aina hiyo.