.
29th May, 2021
Matumaini ya timu ya KCB kumaliza katika nafasi ya kwanza na kufuzu kucheza michuano ya klabu bingwa barani afrika yanaendelea kulowa maji. Hii ni baada ya timu hiyo kulazwa goli moja bila jibu na Sofapaka kwenye mechi ya ligi kuu iliyochezwa ugani Ruaraka Nairobi. Shuti la mbali la kiungo Lawrence Juma limewapa batoto ba mungu ushindi huo muhimu. Kwingineko Nairobi City Stars imelaza Kariobangi Sharks magoli mawili kwa moja.