11th May, 2021
Maelfu ya wanafunzi wanapoendeleaa kusherehekea matokeo bora ya mtihani wa kitaifa wa KCSE, kunao baadhi ambao japo wamefanya vyema, safari yao ya masomo imekuwa yenye tabu tele. Mvulana mmoja kwa jina Moses John kutoka shule ya upili ya Maranda katika kaunti ya Siaya ambaye hana uwezo wa kuona alijifunza kutumia mashine maalum mwaka mmoja tu kabla ya kufanya mtihani wake na akapata alama ya A?. Simulizi yake ni sawa na ya Mariana Wanjiru kutoka mtaa duni wa Kiamaiko Mathare hapa jijini nairobi ambaye awali familia yake ilikuwa ya kurandaranda mitaani lakini baada ya wahisani kugharamia masomo yake katika shule ya upili ya Precious Blood Riruta ana kila sababu ya kutabasamu baada ya kupata alama ya A? pia.