.
21st April, 2021
Makataa ya siku saba ya kupendekezwa kwa majina ya watu saba watakaoteuliwa kwenye jopo la kuwapiga msasa wawaniaji ukamishna wa IEBC imekamilika. Hii inafuatia tangazo la rais kuwa nafasi hizo sasa ziwazi. Hata hivyo kufikia jioni hii ni chama cha mawakili, LSK pekee kilichoweka jina la mteule wake wazi, tume ya huduma za bunge, PSC na muungano wa madhehebu zikisalia kimya. Tume ya IEBC imekuwa na makamishna watatu tu baada ya wanne kuondoka mwaka 2017 na 2018.