.
23rd December, 2020
Mama mmoja mwenye umri wa miaka thelathini na tatu amefariki baada ya kutumbukia baharini pamoja na mwanae na gari walimokuwa wakisafiria katika eneo la kibarani kaunti ya Mombasa. Japo mwanae alinusurika kifo kwa kuogelea kifo cha Winnie Achieng bilashaka kinaleta kumbukumbu ya mkasa wa kivuko cha likoni hiyo mwaka jana ambapo mama Miriam Kighenda pamoja na mwanae walitumbukia baharini na kupatikana tu baada ya majuma matatu.