.
28th March, 2018
Mkufunzi wa timu ya taifa ya raga ya wachezaji saba Innocent Simiyu pomoja na mkufunzi wa kina dada Kevin Wambua wametaja vikosi vitakavyoshiriki mashindano ya Jumuiya ya Madola mwezi ujao pamoja na mikondo ya Msururu wa raga ya dunia Hong Kong na Singapore kwa wanaume. Wengi watasubiri kuona endapo kina dada wa kenya watafuzu miongoni mwa timu kuu kwenye msururu wa mwaka 2018 huku shujaa ikiwa na ari ya kutwaa medali.