Wanariadha Wang'aa jijini London
24th April, 2016
Wanariadha kutoka Kaunti za Elgeiyo Marakwet, Nandi na Uasin Gishu walikusanyika mjini Eldoret ili kufuatilia mbio za London ambapo Wakenya walikuwa wamepigiwa upatu kung’aa, ummati huo ulijumuisha wanariadha waliostaafu na pia wale ambao bado wanajihusisha katika mashindano tofauti huku wasiwasi ukidhihirika wazi haswa pale wanariadha wa uhabeshi walipoonekana kuleta upinzani. Lakini baada ya muda wa saa mbili, wasiwasi uligeuka na kuwa vifijo, shangwe na nderemo pale Eliud Kipchoge na Jemima Sumgong walipofika kwenye utepe wa kwanza na kunyakua ushindi upande wa wanaume na wanawake mtawalia.