Viongozi kutoka Bonde la Ufa hawataki Kenya kujiusisha na mahakama ya ICC
17th April, 2016
Viongozi kutoka Bonde la Ufa wameunga mkono kauli ya Rais Uhuru Kenyatta kwamba hakuna mkenya yeyote ambaye atawahi kwenda katika mahakama ya ICC katika siku za usoni. Vile vile viongozi hao wamewasuta viongozi wa cord kwa kutumia mkutano wao kuwachochea wakenya ilhali wao kama jamii tayari wamesameheana na kuridhiana.