Rais awapongeza wanajeshi Somalia kwenye hotuba yake
31st March, 2016
Kwenye hotuba yake mbele ya wabunge na maseneta, Rais Kenyatta amesifia harakati za majeshi ya kenya nchini Somalia huku akiwaomba wakenya wote kuunga mkono harakati hizo. Aidha kenyatta amekosoa mienendo ya wanasiasa wa upinzani akisema kwamba wafaa kuelewa kwamba jukumu lao si kubadilisha wajibu wa upinzani kuwa mchezo wa sarakasi bali kuhakikisha taifa linaongozwa kwa njia ya kufaa. Aidha kwenye hotuba rais ameelezea baadhi ya ufanisi wa serikali haswa kwenye masuala ya miundo misingi akikiri kwamba amejizatiti kwenye sekta hiyo kukamilisha mipango iliyoanzishwa na serikali ya Rais Mwai Kibaki. Amepigia debe ongezeko la barabara nchini, ujenzi wa reli ya SGR, usambazaji nguvu za umeme hadi mashinani.