Wakristo waadhimisha mwanzo wa wiki takatifu ya Pasaka kwa Jumapili ya Matawi
20th March, 2016
Wakristo kote ulimwenguni wameanza kusherehekea wiki takatifu leo kwa Jumapili ya Matawi. Ni wakati ambao wakristo husherehekea siku za mwisho za yesu kristo kabla ya kifo chake. Hapa jijini Nairobi wakristo walikusanyika makanisani wakiwa na matawi kufungua wiki hii takatifu na kisha kushiriki katika ibada. Jumapili ya matawi huwa ni wakati Yesu alipoingia jurusalemu. Ijumaa njema ikisherehekewa siku aliposulubiwa yesu na kuteseka kwake, kisha kusherehekea jumatatu ya Pasaka.