Shule moja imekua ikivuta mkia kwa miaka mingi inaomba wahisani wainusuru
19th March, 2016
Wanafunzi wa zamani na wa sasa kwenye shule inayovuta mkia kwenye mitihani ya darasa la nane Kaunti Ya Murang’a wametoa wito kwa wahisani kuinusuru. Mbali na kukosa uwanja, vyoo na madarasa yanayofaa, shule ya msingi ya kawanjeru ni vigumu kuifikia kwani hata daraja la kuwezesha wanafunzi kuvuka mto kwenda shuleni halipo. Alama yao ya juu zaidi ya jumla imekuwa 197 tu kwa 500 kwa miaka mitatu iliyopita.