Timu ya Samurai yashinda makala ya 20 ya mashindano ya raga ya Safari Sevens
5th October, 2015
Timu ya Samurai ndio mabingwa wa makala ya 20 ya mashindano ya raga ya Safari Sevens yaliyoandaliwa nchini. Samurai walipata ushindi wa alama 20-19 dhidi ya shujaa ya Kenya kwenye mechi iliyokuwa na upinzani mkali.