Wawakilishi wa wadi Nakuru warushiana makonde kwenye kikao
10th March, 2015
Wawakilishi wa wadi kwenye bunge la Nakuru alasiri ya leo wamerushiana makonde kwenye kikao kufuatia mzozo wa kiongozi wa wengi kwenye bunge hilo. Shughuli zilisambaratishwa katika vikao vitatu mfululizo pale wawakilishi wanaompinga spika Susan Kihika walipoteta kuhusu mapendekezo ya kubadilisha baadhi ya kanuni za bunge, wakidai kuwa marekebisho hayo yanalenga kuwahujumu wale wanaomuunga alikuwa kiongozi wa wengi George Mwaura Njenga.