Chinua Achebe aaga dunia
22nd March, 2013
Mwandishi mashuhuri wa riwaya nchini Nigeria,Chinua Achebe amefariki. Achebe mmoja wa magwiji wa afrika katika utunzi wa hadithi na riwaya ambaye sifa zake zimeenea kote duniani alifariki akiwa na umri wa miaka 82.kitabu chake cha kwanza “Things fall apart” kilichotoa sura kamili ya athari za ukoloni afrika kilitafsiriwa katika lugha zaidi ya 50 na kiliuza nakala milioni kumi.vitabu vyake havikuwakalia vyema viongozi wengi wa afrika, kwani hakuwasaza kwa utawala wa kimla na uongozi mbaya. Raia huyu wa nigeria alikuwa akiishi nchini marekani tangu mwaka wa 1990, kufuatia majeraha aliyopata katika ajali ya barabarani. Mwaka uliopita achebe alichapisha kitabu cha maisha yake akiratibu zaidi vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini nigeria, vilivyojulikana kama“biafra war”. Katika uhai wake achebe alikataa kupokea tuzo kubwa za heshima za nigeria, akisema nigeria imegeuzwa kuwa himaya ya ufisadi na vurugu. Katika risala zake za rambi rambi, rais mstaafu daniel moi alisema kupitia fasihi zake, a