.
24th January, 2022
Familia moja kutoka kaunti ya Wajir inalilia haki baada ya mpendwa wao kuuawa kinyama na mwili wake kutupwa katika eneo la Kolol katika Kaunti ya Elgeyo Marakwet.
Kwa mujibu wa familia hiyo, Abdirahim Adow Abdulahi alikuwa Afisa wa Polisi wa Idara ya Upelelezi mwenye cheo cha Konstebo na alikuwa akifanya kazi katika Kituo cha polisi cha Itabwa Mugoya katika kaunti ya Embu.
Wanasema mauaji yake yametokea wakati alipokuwa akifuatilia kesi kadhaa zinazohusiana na ulanguzi wa dawa za kulevya.
Wakati huo huo polisi walipata miili ya wanaume wawili iliyokuwa imeoza katika barabara kuu ya Kabarnet kuelekea Eldoret.