7th February, 2022
Baadhi ya wafuasi wa chama cha ODM kaunti ya Busia wamemsuta gavana wa Kakamega Wycliffe Oparanya wakidai anaingilia maswala ya chama hicho katika kaunti hiyo kwa kuonekana kuegemea upande wa aliyekuwa mbunge wa Funyula Paul Otuoma. Wafuasi hao wanamtaka Oparanya kusita kuingilia siasa za ni nani anapaswa kupewa tiketi ya chama hicho kuwania ugavana wa kaunti ya Busia bila kutumia njia za mkato.