7th February, 2022
Kuna uwezekano zoezi la mchujo wa chama cha ODM na kile cha Jubilee ambavyo vinaunga vuguvugu la Azimio la Umoja litafanyika kwa wakati mmoja. Kulingana na mkurugenzi wa chaguzi wa chama cha ODM Junet Mohammed, uhusiano wao na chama cha Jubilee utaimarishwa ili kuboresha vyama hivyo viwili kabla ya uchaguzi mkuu wa mwezo Agosti. Aidha Junet amekiri kwamba bado hawajatia mkataba na chama cha jubilee ili kuhakikisha kwamba wana lengo moja.