7th February, 2022
Viongozi kaunti ya Samburu wamewahusisha wakazi wa eneo la Pura katika kutafuta amani, wakati huu visa vya wizi wa mifugo pamoja na kulipisha kisasi vimeongezeka katika eneo hilo. Hatua hii inawadia baada ya watu wanne miongoni mwao OCS wa kituo cha polisi cha Maralal pamoja na afisa mwingine wa polisi kuuawa kwa kupigwa risasi na majangili kwenye matukio tofauti yaliyotokea mwezi Desemba mwaka jana.