19th October, 2021
Kaunti ya Migori inajivunia kuwa na utoshelezo wa chakula licha ya changamoto ambazo wakulima wamekabiliwa nazo kutokana na athari za janga la korona, mfumko wa bei ya pembejeo na mabadiliko ya hali ya anga ambayo imekuwa vigumu kutabiri. Haya ni kwa mujibu wa waziri wa kilimo kaunti hiyo Valentine Ogongo. Wakati uo huo, mkurugenzi wa masuala ya kilimo kaunti hiyo Florence Anyango amesisitizia umuhimu wa kuwahamasisha wakulima kuhusu umuhimu wa kuhakikisha kuna utoshelezo wa chakula na lishe bora katika jamii.