6th May, 2021
Mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa jinai ICC hatimaye imemhukumu kifungo cha miaka ishirini na mitano kiongozi wa zamani wa waasi nchini Uganda wa Lord’s resistance army lra Dominic Ongwen. Ongwen anayefahamika kama white ant, alipatikana na zaidi ya makosa 60 yakiwa ni pamoja na uhalifu dhidi ya binadamu na uhalifu wa kivita.