25th October, 2021
Familia ya Agnes Wanjiru, mwanamke aliyeuwawa na mwanajeshi wa Uingereza takriban mwongo mmoja uliopita sasa inataka serikali ya Kenya na Uingereza kumchukulia hatua mwanajeshi huyo. Hii ni baada ya taarifa kuibuka kuwa mwanajeshi huyo alikiri kumuua wanjiru na kisha kuutupa mwili wake ndani ya pipa la maji taka katika hoteli ya lions court mjini nanyuki mwaka 2012.