.
25th October, 2021
Mabondia wa Kenya wanaendelea kujiandaa jijini Belgrade nchini Serbia. Kenya ina zaidi ya kikosi cha mabondia 30 ambao wakufunzi wana imani watafanya vyema katika mashindano haya ya dunia. Kati ya mabondia wa Kenya tajika ni bondia Nick Okoth aliyeshiriki katika mashindano ya olimpiki jijini Tokyo nchini Japan na japo hakifanya vyema katika mashindano hayo ana imani kwamba amejitayarisha vilivyo kukabiliana na upinzani ujao.